Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 14:1-7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Mpumbavu* husema moyoni mwake:

      “Hakuna Yehova.”+

      Matendo yao yamepotoka, na shughuli zao zinachukiza;

      Hakuna yeyote anayetenda mema.+

       2 Lakini Yehova anawatazama wanadamu kutoka mbinguni

      Ili aone ikiwa kuna yeyote aliye na ufahamu, ikiwa kuna yeyote anayemtafuta Yehova.+

       3 Wote wamegeuka kando;+

      Wote wamepotoka.

      Hakuna yeyote anayetenda mema,

      Hakuna hata mmoja.

       4 Je, hakuna mtenda maovu yeyote anayeelewa?

      Wanawala watu wangu kana kwamba wanakula mkate.

      Hawamwiti Yehova.

       5 Lakini watajawa na hofu kubwa,+

      Kwa maana Yehova yuko pamoja na kizazi cha waadilifu.

       6 Ninyi waovu hujaribu kuharibu mipango ya mtu wa hali ya chini,

      Lakini Yehova ni kimbilio lake.+

       7 Laiti wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+

      Yehova anapowakusanya tena watu wake waliotekwa,

      Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi.

  • Waroma 3:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwanadamu mwadilifu, hakuna hata mmoja;+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki