Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Samweli 7:12-15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Siku zako zitakapokwisha+ nawe ufe na kuzikwa pamoja na mababu zako, ndipo nitakapomwinua mzao wako* baada yako, mwana wako mwenyewe,* nami nitauimarisha kabisa ufalme wake.+ 13 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu,+ nami nitakiimarisha kabisa kiti cha ufalme wake milele.+ 14 Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu.+ Atakapokosea, nitamkaripia kwa fimbo ya wanadamu na kwa viboko vya wana wa binadamu.*+ 15 Upendo wangu mshikamanifu hautaondolewa kwake kama nilivyouondoa kwa Sauli,+ niliyemwondoa kutoka mbele yako.

  • Zaburi 132:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Yehova amemwapia Daudi;

      Kwa hakika hatakosa kutimiza neno lake:

      “Mmoja wa wazao wako,*

      Nitamfanya aketi kwenye kiti chako cha ufalme.+

  • Isaya 55:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Tegeni sikio na mje kwangu.+

      Sikilizeni, nanyi mtaendelea* kuwa hai,

      Nami nitafanya agano la milele pamoja nanyi bila kusita+

      Kulingana na matendo ya upendo mshikamanifu kwa Daudi, ambayo ni ya uaminifu.*+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki