-
Kutoka 16:12-15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 “Nimesikia manung’uniko ya Waisraeli.+ Waambie hivi: ‘Jioni kabla ya giza kuingia* mtakula nyama, na asubuhi mtashiba mikate,+ nanyi mtajua kwa hakika kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu.’”+
13 Basi jioni hiyo kware wakaja na kufunika kambi,+ na asubuhi utando wa umande ulizunguka kambi yote. 14 Utando huo wa umande ulipotoweka, kitu laini, kinachovunjikavunjika,+ kitu laini kama theluji, kilienea kwenye ardhi nyikani. 15 Waisraeli walipokiona, walianza kuulizana: “Ni nini hiki?” kwa maana hawakujua kilikuwa nini. Musa akawaambia: “Ni mkate ambao Yehova amewapa uwe chakula chenu.+
-