-
Yeremia 25:31-33Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
31 ‘Kelele zitasikika mpaka kwenye miisho ya dunia,
Kwa maana Yehova ana kesi dhidi ya mataifa.
Yeye binafsi atawahukumu wanadamu wote.*+
Naye atawaangamiza waovu kwa upanga,’ asema Yehova.
32 Yehova wa majeshi anasema hivi:
‘Tazameni! Msiba unaenea kutoka taifa mpaka taifa,+
Na tufani kubwa itaachiliwa kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+
33 “‘Na wale ambao Yehova atawaua siku hiyo watatapakaa kutoka mwisho mmoja wa dunia mpaka mwisho wa pili wa dunia. Hawataombolezewa, wala kukusanywa wala kuzikwa. Watakuwa kama mbolea juu ya ardhi.’
-