Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 21:7-9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Wakamleta huyo punda na mwanapunda wake, kisha wakatandika juu yao mavazi yao ya nje, naye akayakalia.+ 8 Wengi katika umati wakatandaza mavazi yao ya nje barabarani,+ na wengine wakakata matawi ya miti na kuyatandaza barabarani. 9 Isitoshe umati uliomtangulia na wale waliomfuata waliendelea kupaza sauti: “Tunaomba umwokoe, Mwana wa Daudi!+ Amebarikiwa yule anayekuja katika jina la Yehova!*+ Tunaomba umwokoe, katika vilele vilivyo juu!”+

  • Mathayo 23:39
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 39 Kwa maana ninawaambia, tangu sasa hamtaniona tena mpaka mtakaposema, ‘Amebarikiwa yule anayekuja katika jina la Yehova!’”*+

  • Marko 11:7-10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Wakampelekea Yesu huyo mwanapunda,+ wakatandika mavazi yao ya nje juu yake, naye akaketi juu yake.+ 8 Pia, wengi wakatandaza mavazi yao ya nje barabarani, lakini wengine wakatandaza matawi ya miti waliyokata katika mashamba.+ 9 Watu waliokuwa mbele na wale waliofuata nyuma wakaendelea kupaza sauti: “Tunaomba umwokoe!+ Amebarikiwa yule anayekuja katika jina la Yehova!*+⁠ 10 Umebarikiwa Ufalme unaokuja wa baba yetu Daudi!+ Tunaomba umwokoe, katika vilele vilivyo juu!”

  • Luka 19:37, 38
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 37 Alipokaribia tu barabara ya kushuka Mlima wa Mizeituni umati wote wa wanafunzi ukaanza kushangilia na kumsifu Mungu kwa sauti kubwa kwa sababu ya matendo yote yenye nguvu ambayo walikuwa wameona, 38 na kusema: “Amebarikiwa yule anayekuja akiwa Mfalme katika jina la Yehova!* Amani mbinguni, na utukufu katika vilele vilivyo juu!”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki