Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nehemia 4:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Sikiliza, Ee Mungu wetu, kwa maana tunadharauliwa;+ na urudishe dharau yao juu ya vichwa vyao wenyewe,+ nawe uwafanye wawe nyara na mateka katika nchi nyingine.

  • Nehemia 6:15, 16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Mwishowe ukuta ulikamilishwa katika siku ya 25 ya mwezi wa Eluli,* kwa muda wa siku 52.

      16 Mara tu maadui wetu wote waliposikia habari hiyo na mataifa yote jirani yalipoona jambo hilo, wakaaibika sana,+ nao wakatambua kwamba kazi hii ilikuwa imefanywa kwa msaada wa Mungu wetu.

  • Esta 6:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Hamani alipomsimulia Zereshi mke wake+ na marafiki zake wote mambo yaliyompata, watu wake wenye hekima na Zereshi mke wake wakamwambia: “Ikiwa Mordekai ambaye umeanza kuanguka mbele yake ni wa uzao wa Kiyahudi,* hutaweza kumshinda; kwa hakika utaanguka mbele yake.”

  • Esta 9:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Wayahudi waliwashambulia kwa upanga maadui wao wote, wakawaua na kuwaangamiza; waliwatendea walivyotaka wale waliowachukia.+

  • Zaburi 137:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Kumbuka, Ee Yehova,

      Mambo ambayo Waedomu walisema siku ambayo Yerusalemu lilianguka:

      “Libomoeni! Libomoeni mpaka kwenye misingi yake!”+

  • Zekaria 12:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Siku hiyo nitafanya Yerusalemu liwe jiwe zito* kwa mataifa yote. Kwa hakika wote watakaolinyanyua watajeruhiwa vibaya;+ na mataifa yote duniani yatakusanyika kupigana na jiji hilo.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki