10 Kwa sababu ya ukatili uliomtendea ndugu yako Yakobo,+
Aibu itakufunika,+
Nawe utaangamia milele.+
11 Siku uliyosimama kando,
Siku ambayo wageni walichukua jeshi lake na kulipeleka utekwani,+
Wageni walipoingia katika lango lake na kugawana Yerusalemu kwa kura,+
Ulitenda kama wao.
12 Hupaswi kucheka siku ambayo ndugu yako anapatwa na maafa,+
Hupaswi kushangilia siku ambayo watu wa Yuda wanaangamia,+
Nawe hupaswi kujigamba sana siku wanayotaabika.
13 Hupaswi kuingia katika lango la watu wangu siku wanayopatwa na msiba,+
Hupaswi kuwacheka siku wanayopatwa na msiba,
Nawe hupaswi kuchukua mali yao siku wanayopatwa na msiba.+