Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 27:41, 42
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 41 Hata hivyo, Esau akawa na chuki kali dhidi ya Yakobo kwa sababu ya baraka ambayo baba yake alikuwa amempa,+ na Esau akawa akisema moyoni mwake: “Siku za kumwombolezea baba yangu zinakaribia.+ Zitakapokwisha nitamuua Yakobo ndugu yangu.” 42 Rebeka alipoambiwa maneno ya Esau mwana wake mkubwa, mara moja akaagiza Yakobo mwana wake mdogo aitwe, akamwambia: “Tazama! Esau ndugu yako anapanga kukuua ili kulipiza kisasi.*

  • Hesabu 20:20, 21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Lakini bado akasema, “Hamtapita.”+ Ndipo mfalme wa Edomu akatoka ili kumshambulia akiwa na watu wengi na jeshi lenye nguvu.* 21 Basi mfalme wa Edomu akakataa kuwaruhusu Waisraeli wapite katika eneo lake; kwa hiyo Waisraeli wakageuka na kumwacha.+

  • Zaburi 83:4-6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Wanasema: “Njooni, acheni tuwaangamize wakiwa taifa,+

      Ili jina la Israeli lisikumbukwe tena kamwe.”

       5 Kwa umoja wanatunga mbinu;*

      Wameungana* dhidi yako+—

       6 Mahema ya Edomu na Waishmaeli, Moabu+ na Wahagri,+

  • Zaburi 137:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Kumbuka, Ee Yehova,

      Mambo ambayo Waedomu walisema siku ambayo Yerusalemu lilianguka:

      “Libomoeni! Libomoeni mpaka kwenye misingi yake!”+

  • Yoeli 3:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Lakini Misri itakuwa ukiwa,+

      Na Edomu itakuwa nyika iliyo ukiwa,+

      Kwa sababu ya ukatili waliowatendea watu wa Yuda,+

      Katika nchi yao walimwaga damu isiyo na hatia.+

  • Amosi 1:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Yehova anasema hivi:

      ‘Kwa sababu ya maasi matatu ya Edomu,+ na hata manne, sitabadili uamuzi wangu,

      Kwa sababu alimfuatia kwa upanga ndugu yake mwenyewe,+

      Na kwa sababu alikataa kuonyesha rehema;

      Katika hasira yake anaendelea kuwararuararua bila huruma,

      Na bado anaendelea kuwakasirikia vikali.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki