7 Lakini Yehova akamwambia Samweli: “Usitazame sura yake wala urefu wake,+ kwa maana nimemkataa. Kwa kuwa Mungu haoni kama mwanadamu anavyoona, kwa maana mwanadamu huona kinachoonekana kwa macho, lakini Yehova huona ndani ya moyo.”+
3 “Nakusihi, Ee Yehova, tafadhali, kumbuka jinsi ambavyo nimetembea mbele zako kwa uaminifu na kwa moyo kamili, nami nimetenda mambo mema machoni pako.”+ Kisha Hezekia akaanza kulia sana na kububujikwa na machozi.
17 Ee Mungu wangu, najua vizuri kwamba wewe huuchunguza moyo,+ na kwamba unapendezwa na utimilifu.*+ Kwa unyoofu wa moyo wangu, nimetoa kwa hiari vitu hivi vyote, nami nimefurikwa na shangwe kuwaona watu wako walio hapa wakikutolea matoleo ya hiari.