-
Yoshua 7:24, 25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 Yoshua na Waisraeli wote wakamchukua Akani+ mwana wa Zera, zile fedha, lile vazi rasmi maridadi, na kile kipande cha dhahabu,+ pamoja na wanawe, binti zake, ng’ombe dume wake, punda wake, kondoo na mbuzi wake, hema lake, na vitu vyake vyote, wakavileta katika Bonde la* Akori.+ 25 Yoshua akasema: “Kwa nini umetuletea msiba?*+ Leo Yehova atakuletea msiba.” Ndipo Waisraeli wote wakawapiga mawe,+ kisha wakawateketeza kwa moto.+ Naam, waliwapiga mawe wote.
-
-
Esta 9:24, 25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 Kwa maana Hamani+ mwana wa Hamedatha Mwagagi,+ adui ya Wayahudi wote, alikuwa amepanga njama ya kuwaangamiza Wayahudi,+ na alikuwa amepiga Puri,+ yaani, Kura, ili kuwatisha na kuwaangamiza. 25 Lakini Esta alipokuja mbele ya mfalme, mfalme alitoa agizo lililoandikwa hivi:+ “Njama yake mbaya dhidi ya Wayahudi+ na irudi juu ya kichwa chake mwenyewe”; nao wakamtundika yeye pamoja na wanawe mtini.+
-