6 Mwendee chungu, ewe mvivu;+
Zichunguze njia zake uwe na hekima.
7 Ingawa hana kamanda, ofisa, au mtawala,
8 Yeye hutayarisha chakula chake wakati wa kiangazi,+
Na kukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
9 Ewe mvivu, utaendelea kulala hapo mpaka lini?
Utaamka lini kutoka katika usingizi wako?
10 Lala kidogo, sinzia kidogo,
Kunja mikono kidogo ili upumzike,+
11 Na umaskini wako utakuja kama jambazi,
Na uhitaji wako kama mwanamume mwenye silaha.+