9 Shangilia, ewe kijana, wakati ungali kijana, na moyo wako ushangilie siku za ujana wako. Fuata njia za moyo wako na uende mahali ambapo macho yako yanakuongoza; lakini ujue kwamba Mungu wa kweli atakuhukumu* kwa sababu ya mambo hayo yote.+
36 Ninawaambia kwamba katika Siku ya Hukumu watu watatoa hesabu+ kuhusu kila neno lisilofaa wanalosema; 37 kwa maneno yako utatangazwa kuwa mwadilifu, na kwa maneno yako utahukumiwa.”
31 Kwa sababu ameweka siku ambayo anakusudia kuihukumu+ kwa uadilifu dunia inayokaliwa kupitia mwanamume ambaye amemweka rasmi, naye ametoa uhakikisho kamili kwa watu wote kwa kuwa amemfufua kutoka kwa wafu.”+
10 Kwa maana lazima sisi sote tusimame* mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apate malipo kulingana na mambo aliyotenda akiwa katika mwili, yawe mema au mabaya.*+