-
Mhubiri 5:18, 19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Hili ndilo jambo ambalo nimeona ni jema na linafaa: kwamba mtu anapaswa kula na kunywa na kufurahia kazi yote ngumu+ anayofanya kwa jasho chini ya jua katika siku chache za maisha alizopewa na Mungu wa kweli, kwa maana hiyo ndiyo thawabu yake.*+ 19 Pia, Mungu wa kweli anapompa mtu utajiri na mali+ pamoja na uwezo wa kufurahia vitu hivyo, anapaswa kuchukua thawabu yake* na kushangilia katika kazi yake ngumu. Hiyo ndiyo zawadi kutoka kwa Mungu.+
-