-
2 Wafalme 17:13, 14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Yehova aliwaonya Waisraeli na watu wa Yuda tena na tena kupitia manabii wake wote na kila mwonaji,+ akisema: “Geukeni na kuacha njia zenu ovu!+ Shikeni amri zangu na maagizo yangu kulingana na sheria yote niliyowaamuru mababu zenu na ambayo niliwapa kupitia watumishi wangu manabii.” 14 Lakini hawakusikiliza, nao wakaendelea kuwa wakaidi kama* mababu zao ambao hawakudhihirisha imani katika Yehova Mungu wao.+
-
-
2 Mambo ya Nyakati 36:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Yehova Mungu wa mababu zao aliendelea kuwaonya kupitia wajumbe wake, aliwaonya tena na tena, kwa sababu aliwahurumia watu wake na makao yake. 16 Lakini waliendelea kuwadhihaki wajumbe wa Mungu wa kweli,+ wakadharau maneno yake+ na kuwakejeli manabii wake,+ mpaka ghadhabu ya Yehova ilipokuja dhidi ya watu wake,+ hivi kwamba hawangeweza kuponywa.
-