-
2 Wafalme 16:8, 9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Kisha Ahazi akachukua fedha na dhahabu iliyokuwa katika nyumba ya Yehova na katika hazina za nyumba ya mfalme,* akampelekea mfalme wa Ashuru kama rushwa.+ 9 Mfalme wa Ashuru akakubali ombi lake, naye akapanda kwenda Damasko na kuliteka jiji hilo na kuwapeleka watu wake uhamishoni huko Kiri,+ akamuua Resini.+
-
-
Isaya 8:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Ndipo nikalala na* yule nabii wa kike,* naye akapata mimba na baada ya muda akazaa mwana.+ Kisha Yehova akaniambia: “Mwite jina Maher-shalal-hash-bazi, 4 kwa maana kabla mvulana huyo hajajua jinsi ya kuita, ‘Baba yangu!’ na ‘Mama yangu!’ mali za Damasko na nyara za Samaria zitachukuliwa mbele ya mfalme wa Ashuru.”+
-