Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 15:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Katika siku za utawala wa Mfalme Peka wa Israeli, Mfalme Tiglath-pileseri+ wa Ashuru alivamia na kuteka Iyoni, Abel-beth-maaka,+ Yanoa, Kedeshi, Hasori, Gileadi,+ na Galilaya,+ nchi yote ya Naftali,+ akawapeleka wakaaji wa maeneo hayo uhamishoni kule Ashuru.+

  • 2 Wafalme 16:8, 9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Kisha Ahazi akachukua fedha na dhahabu iliyokuwa katika nyumba ya Yehova na katika hazina za nyumba ya mfalme,* akampelekea mfalme wa Ashuru kama rushwa.+ 9 Mfalme wa Ashuru akakubali ombi lake, naye akapanda kwenda Damasko na kuliteka jiji hilo na kuwapeleka watu wake uhamishoni huko Kiri,+ akamuua Resini.+

  • 2 Wafalme 17:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mfalme wa Ashuru aliliteka jiji la Samaria.+ Kisha akawapeleka Waisraeli uhamishoni+ kule Ashuru na kuwaweka katika eneo la Hala na Habori kando ya mto Gozani+ na katika majiji ya Wamedi ili waishi humo.+

  • Isaya 7:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Kwa maana kabla ya mvulana huyo kujua jinsi ya kukataa lililo baya na kuchagua lililo jema, nchi ya wale wafalme wawili mnaowahofu itaachwa kabisa.+

  • Isaya 17:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Tangazo dhidi ya Damasko:+

      “Tazama! Damasko halitakuwa jiji tena,

      Nalo litakuwa rundo la magofu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki