Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 2:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Na watu wa mataifa mengi wataenda na kusema:

      “Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova,

      Kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+

      Naye atatufundisha njia zake,

      Nasi tutatembea katika vijia vyake.”+

      Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,

      Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.+

       4 Atatekeleza hukumu miongoni mwa mataifa

      Na kunyoosha* mambo kuhusiana na watu wengi.

      Watafua panga zao ziwe majembe ya plau

      Na mikuki yao iwe miundu.+

      Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa lingine,

      Wala hawatajifunza vita tena kamwe.+

  • Isaya 11:6-9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Mbwamwitu atakaa pamoja na mwanakondoo kwa muda fulani,+

      Na chui atalala pamoja na mwanambuzi,

      Na ndama na simba* na mnyama aliyenoneshwa wote watakuwa pamoja;*+

      Na mvulana mdogo atawaongoza.

       7 Ng’ombe na dubu watakula pamoja,

      Na watoto wao watalala pamoja.

      Simba atakula majani kama ng’ombe dume.+

       8 Na mtoto anayenyonya atacheza juu ya shimo la swila,

      Na mtoto aliyeachishwa kunyonya atatia mkono wake juu ya shimo la nyoka mwenye sumu.

       9 Hawatasababisha madhara yoyote+

      Wala uharibifu wowote katika mlima wangu wote mtakatifu,+

      Kwa maana kwa hakika dunia itajaa ujuzi kumhusu Yehova

      Kama maji yanavyoifunika bahari.+

  • Mika 4:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Na mataifa mengi yataenda na kusema:

      “Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova

      Na kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+

      Naye atatufundisha njia zake,

      Nasi tutatembea katika vijia vyake.”

      Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,

      Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki