- 
	                        
            
            Isaya 2:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
3 Na watu wa mataifa mengi wataenda na kusema:
“Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova,
Kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+
Naye atatufundisha njia zake,
Nasi tutatembea katika vijia vyake.”+
Watafua panga zao ziwe majembe ya plau
Na mikuki yao iwe miundu.+
Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa lingine,
Wala hawatajifunza vita tena kamwe.+
 
 - 
                                        
 
- 
	                        
            
            Isaya 11:6-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
6 Mbwamwitu atakaa pamoja na mwanakondoo kwa muda fulani,+
Na chui atalala pamoja na mwanambuzi,
Na ndama na simba* na mnyama aliyenoneshwa wote watakuwa pamoja;*+
Na mvulana mdogo atawaongoza.
7 Ng’ombe na dubu watakula pamoja,
Na watoto wao watalala pamoja.
Simba atakula majani kama ng’ombe dume.+
8 Na mtoto anayenyonya atacheza juu ya shimo la swila,
Na mtoto aliyeachishwa kunyonya atatia mkono wake juu ya shimo la nyoka mwenye sumu.
 
 -