Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 4:13-16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Isitoshe, baada ya kuondoka Nazareti, akaenda kukaa Kapernaumu+ kando ya bahari katika wilaya za Zabuloni na Naftali, 14 ili kutimiza maneno haya yaliyosemwa kupitia nabii Isaya, aliyesema: 15 “Ewe nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kando ya barabara ya bahari, ng’ambo ya Yordani, katika Galilaya ya mataifa! 16 Watu wanaokaa katika giza waliona nuru kuu, na wale wanaokaa katika eneo la kivuli cha kifo, nuru+ iliwaangazia.”+

  • Luka 1:78, 79
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 78 kwa sababu ya huruma nyororo za Mungu wetu. Kwa huruma hizo tutapata mapambazuko kutoka juu, 79 ili kuwapa nuru wale wanaokaa gizani na katika kivuli cha kifo+ na kuongoza hatua zetu kwenye njia ya amani.”

  • Luka 2:30-32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 kwa sababu macho yangu yameona njia yako ya kuleta wokovu+ 31 ambayo umetayarisha machoni pa watu wote,+ 32 nuru+ ya kuondoa kitambaa* kwa mataifa+ na utukufu wa watu wako Israeli.”

  • Yohana 1:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Nuru ya kweli inayowaangazia watu wa aina zote ilikuwa karibu kuja ulimwenguni.+

  • Yohana 8:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 12 Kisha Yesu akawaambia tena: “Mimi ndiye nuru ya ulimwengu.+ Yeyote anayenifuata hatatembea kamwe gizani, bali atakuwa na nuru+ ya uzima.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki