Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 32:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Kwa maana mnara wenye ngome umeachwa;

      Jiji lenye kelele limeachwa.+

      Ofeli+ na mnara wa mlinzi vimebaki ukiwa daima,

      Mahali panapopendwa na punda wa mwituni,

      Malisho ya mifugo,+

  • Yeremia 9:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Nitalifanya Yerusalemu kuwa rundo la mawe,+ mapango ya mbwamwitu,+

      Nami nitayafanya majiji ya Yuda yawe ukiwa, bila mkaaji.+

  • Maombolezo 1:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Barabara zinazoelekea Sayuni zinaomboleza, kwa sababu hakuna yeyote anayekuja kwenye sherehe.+

      Malango yake yote yamebaki ukiwa;+ makuhani wake wanalia kwa uchungu.

      Mabikira* wake wanaomboleza, naye analia kwa maumivu makali.

  • Maombolezo 2:8, 9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Yehova ameazimia kuuharibu ukuta wa binti ya Sayuni.+

      Ameinyoosha kamba ya kupimia.+

      Hajauzuia mkono wake usilete maangamizi.*

      Naye husababisha maboma na kuta ziomboleze.

      Zote pamoja zimedhoofishwa.

      ט [Teth]

       9 Malango yake yamezama chini ardhini.+

      Ameyaharibu na kuyavunja makomeo yake.

      Mfalme wake na wakuu wake wako miongoni mwa mataifa.+

      Hakuna sheria;* hata manabii wake hawapati maono kutoka kwa Yehova.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki