Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 25:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Atameza* kifo milele,+

      Na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atafuta kabisa machozi katika nyuso zote.+

      Shutuma ya watu wake ataiondoa katika dunia yote,

      Kwa maana Yehova mwenyewe amesema hayo.

  • Hosea 13:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Nitawakomboa kutoka katika nguvu za Kaburi;*

      Nitawaokoa kutoka katika kifo.+

      Ewe Kifo, yako wapi maumivu yako makali?*+

      Ewe Kaburi, yako wapi maangamizi yako?+

      Macho yangu yatazuiwa yasione huruma.

  • Marko 12:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Lakini kuhusu kufufuliwa kwa wafu, je, hamkusoma katika kitabu cha Musa, simulizi kuhusu kile kichaka cha miiba kwamba Mungu alimwambia: ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo’?+

  • Yohana 5:28, 29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Msishangazwe na jambo hili, kwa maana saa inakuja ambayo wote walio katika makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake+ 29 na kutoka, wale waliotenda mema kwenye ufufuo wa uzima, na wale waliozoea kutenda maovu kwenye ufufuo wa hukumu.+

  • Yohana 11:24, 25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Martha akamwambia: “Ninajua atafufuka katika ufufuo+ siku ya mwisho.” 25 Yesu akamwambia: “Mimi ndiye ufufuo na uzima.+ Yule anayeniamini, hata akifa, ataishi tena;

  • Matendo 24:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Nami nina tumaini kwa Mungu, tumaini ambalo watu hawa pia wanatazamia, kwamba kutakuwa na ufufuo+ wa waadilifu na wasio waadilifu pia.+

  • 1 Wakorintho 15:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Kwa kuwa kifo kilikuja kupitia mwanadamu,+ ufufuo wa wafu pia unakuja kupitia mwanadamu.+

  • 1 Wathesalonike 4:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Kwa maana ikiwa tunaamini kwamba Yesu alikufa na kufufuliwa,+ vivyo hivyo Mungu atawafufua wale ambao wamelala usingizi katika kifo kupitia Yesu.+

  • Ufunuo 20:12, 13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Nami nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wakiwa wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme, na vitabu vya kukunjwa vikafunguliwa. Lakini kitabu kingine cha kukunjwa kikafunguliwa; hicho ni kitabu cha uzima.+ Wafu wakahukumiwa kutokana na yale mambo yaliyoandikwa katika vile vitabu kulingana na matendo yao.+ 13 Na bahari ikawatoa wafu waliokuwa ndani yake, na kifo na Kaburi* vikawatoa wafu waliokuwa ndani yake, nao wakahukumiwa kila mmoja kulingana na matendo yake.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki