Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 4:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Siku hiyo kile ambacho Yehova atachipusha kitakuwa kizuri sana na chenye utukufu, na mazao ya nchi yatakuwa kitu cha kujivunia na urembo kwa ajili ya waokokaji wa Israeli.+

  • Isaya 27:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Siku zinazokuja Yakobo atatia mizizi,

      Israeli atachanua maua na kuchipuka,+

      Nao watajaza mazao katika nchi.+

  • Isaya 35:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Wakati huo kilema ataruka kama paa,+

      Na ulimi wa bubu utapiga vigelegele vya shangwe.+

      Kwa maana maji yatabubujika nyikani,

      Na vijito katika jangwa tambarare.

  • Isaya 51:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Kwa maana Yehova atalifariji Sayuni.+

      Ataleta faraja kwa magofu yake yote,+

      Naye ataifanya nyika yake kuwa kama Edeni+

      Na jangwa lake tambarare kama bustani ya Yehova.+

      Kutakuwa na furaha na shangwe ndani yake,

      Kutoa shukrani na nyimbo tamu.+

  • Ezekieli 36:35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Na watu watasema: “Nchi iliyokuwa ukiwa imekuwa kama bustani ya Edeni,+ na majiji yaliyokuwa magofu na yaliyokuwa ukiwa na kubomolewa sasa yana ngome na yanakaliwa na watu.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki