-
Yoshua 10:29, 30Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
29 Kisha Yoshua na Waisraeli wote wakatoka Makeda na kwenda Libna, wakalishambulia jiji la Libna.+ 30 Yehova akalitia pia jiji hilo na mfalme wake+ mikononi mwa Waisraeli, wakalishambulia na kuwaangamiza wakaaji wote kwa upanga, na hakuna yeyote aliyebaki humo. Wakamtendea mfalme wake kama walivyomtendea mfalme wa Yeriko.+
-
-
2 Wafalme 19:8-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Baada ya Rabshake kusikia kwamba mfalme wa Ashuru ameondoka Lakishi,+ alirudi na kumkuta akipigana vita na Libna.+ 9 Ndipo mfalme akasikia maneno haya yakisemwa kumhusu Tirhaka mfalme wa Ethiopia: “Ametoka ili kuja kupigana nawe.” Kwa hiyo akawatuma tena wajumbe+ kwa Hezekia, akisema: 10 “Mwambieni hivi Mfalme Hezekia wa Yuda: ‘Usikubali Mungu wako unayemtumaini akudanganye akisema: “Yerusalemu halitatiwa mikononi mwa mfalme wa Ashuru.”+ 11 Tazama! Umesikia mambo ambayo wafalme wa Ashuru walizitendea nchi zote kwa kuziangamiza.+ Je, ni wewe peke yako utakayeokolewa? 12 Je, miungu ya mataifa yaliyoangamizwa na mababu zangu iliyaokoa mataifa hayo? Gozani, Harani,+ Resefu, na watu wa Edeni waliokuwa Tel-asari wako wapi? 13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, na mfalme wa majiji ya Sefarvaimu, na wa Hena, na wa Iva?’”+
-