Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Samweli 7:16, 17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Nyumba yako na ufalme wako utakuwa salama milele mbele yako; kiti chako cha ufalme kitaimarishwa kabisa milele.”’”+

      17 Nathani akamwambia Daudi maneno hayo yote na maono hayo yote.+

  • 1 Wafalme 2:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Na Yehova atatimiza ahadi aliyotoa kunihusu aliposema hivi: ‘Ikiwa wana wako wataikazia uangalifu njia yao kwa kutembea kwa uaminifu mbele zangu kwa moyo wao wote na kwa nafsi* yao yote,+ hutakosa kamwe mwanamume wa uzao wako atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha Israeli.’+

  • Zaburi 89:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Nimempata Daudi mtumishi wangu;+

      Kwa mafuta yangu matakatifu nimemtia mafuta.+

  • Zaburi 89:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Nitauimarisha uzao wake* milele

      Na kukifanya kiti chake cha ufalme kidumu kama mbingu.+

  • Isaya 9:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Kwa wingi wa utawala wake*

      Na amani, hakutakuwa na mwisho,+

      Kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ na juu ya ufalme wake

      Ili kuuimarisha kabisa+ na kuutegemeza

      Kupitia haki+ na uadilifu,+

      Kuanzia sasa mpaka milele.

      Bidii ya Yehova wa majeshi itafanya hayo.

  • Luka 1:32, 33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Huyo atakuwa mkuu+ naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi,+ na Yehova* Mungu atampa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake,+ 33 naye atatawala akiwa Mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki