-
Yoshua 23:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Lakini kama zilivyotimia ahadi zote nzuri alizowaahidi Yehova Mungu wenu,+ vivyo hivyo Yehova atawaletea misiba yote aliyoahidi* na kuwaangamiza kutoka katika nchi hii nzuri ambayo Yehova Mungu wenu amewapa.+ 16 Mkivunja agano la Yehova Mungu wenu alilowaamuru mshike na mkienda kuabudu miungu mingine na kuiinamia, hasira ya Yehova itawaka dhidi yenu+ nanyi mtaangamia haraka kutoka katika nchi nzuri ambayo amewapa.”+
-