-
Yeremia 21:7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 “‘“Baada ya hayo,” asema Yehova, “Nitamtia Mfalme Sedekia wa Yuda na watumishi wake na watu wa jiji hili—wale watakaookoka ugonjwa hatari, upanga, na njaa kali—mikononi mwa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni, mikononi mwa maadui wao na mikononi mwa wale wanaotaka kuwaua.*+ Atawaua kwa upanga. Hatawasikitikia wala kuwahurumia wala kuwaonyesha rehema yoyote.”’+
-
-
Ezekieli 12:12, 13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Mkuu aliye miongoni mwao atabeba mizigo yake begani na kuondoka kukiwa na giza. Atatoboa shimo ukutani na kuibeba mizigo yake kupitia humo.+ Ataufunika uso wake ili asione chini.’ 13 Nitautandaza wavu wangu juu yake, naye atakamatwa katika wavu wangu wa kuwindia.+ Kisha nitampeleka Babiloni, kwenye nchi ya Wakaldayo, lakini hataiona; naye atafia huko.+
-