-
Ezekieli 8:10, 11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Basi nikaingia na kutazama, nikaona mifano mbalimbali ya viumbe wanaotambaa na wanyama wanaochukiza+ na sanamu zote zinazochukiza* za watu wa nyumba ya Israeli;+ zilikuwa zimechongwa ukutani kuzunguka pande zote. 11 Na wazee 70 wa nyumba ya Israeli walikuwa wamesimama mbele ya vitu hivyo, naye Yaazania mwana wa Shafani+ alikuwa amesimama miongoni mwao. Kila mmoja wao alikuwa na chetezo chake mkononi mwake, na wingu la uvumba lenye manukato lilikuwa likipanda juu.+
-