Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waamuzi 2:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Wakamwacha Yehova na kuabudu Baali na sanamu za Ashtorethi.+

  • Waamuzi 3:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Basi Waisraeli wakatenda maovu machoni pa Yehova, wakamsahau Yehova Mungu wao, na kuabudu Mabaali+ na miti mitakatifu.*+

  • 1 Wafalme 16:30-32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Ahabu mwana wa Omri alikuwa mwovu sana machoni pa Yehova kuliko wote waliomtangulia.+ 31 Na kana kwamba lilikuwa jambo dogo kwake kutembea katika dhambi za Yeroboamu+ mwana wa Nebati, hata alimwoa Yezebeli+ binti ya Ethbaali, mfalme wa Wasidoni,+ akaanza kumwabudu Baali+ na kumwinamia. 32 Isitoshe, alisimamisha madhabahu kwa ajili ya Baali katika nyumba ya Baali+ aliyoijenga* kule Samaria.

  • 1 Wafalme 18:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Na sasa nikusanyie Waisraeli wote kwenye Mlima Karmeli,+ pamoja na manabii 450 wa Baali na manabii 400 wa mti mtakatifu,*+ wanaokula kwenye meza ya Yezebeli.”

  • 2 Wafalme 17:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Yehova aliwaonya Waisraeli na watu wa Yuda tena na tena kupitia manabii wake wote na kila mwonaji,+ akisema: “Geukeni na kuacha njia zenu ovu!+ Shikeni amri zangu na maagizo yangu kulingana na sheria yote niliyowaamuru mababu zenu na ambayo niliwapa kupitia watumishi wangu manabii.”

  • 2 Wafalme 17:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Waliendelea kuacha amri zote za Yehova Mungu wao, nao wakatengeneza sanamu za chuma* za ndama wawili+ na kutengeneza mti mtakatifu,*+ nao wakaliinamia jeshi lote la mbinguni+ na kumwabudu Baali.+

  • Hosea 2:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Nitamfanya awajibike kwa sababu ya siku alizotumia kutoa dhabihu kwa sanamu za Baali,+

      Alipokuwa akijipamba kwa pete zake na mapambo yake na kuwafuatia wapenzi wake,

      Na mimi ndiye aliyenisahau,’+ asema Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki