Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 79:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Wamewapa ndege wa angani maiti za watumishi wako kuwa chakula chao

      Na miili ya washikamanifu wako wamewapa wanyama wa mwituni wa dunia.+

       3 Wamemwaga damu yao kama maji kotekote Yerusalemu,

      Na hakuna aliyebaki wa kuwazika.+

  • Isaya 5:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Ndiyo sababu hasira ya Yehova inawaka dhidi ya watu wake,

      Naye ataunyoosha mkono wake dhidi yao na kuwapiga.+

      Milima itatetemeka,

      Na maiti zao zitakuwa kama takataka barabarani.+

      Kwa sababu ya hayo yote, hasira yake haijapoa,

      Lakini mkono wake bado umenyooshwa ili kupiga.

  • Yeremia 7:33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 Na maiti za watu hawa zitakuwa chakula cha ndege wa angani na cha wanyama wa duniani, na hakuna mtu atakayewafukuza.+

  • Yeremia 9:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Sema, ‘Yehova anasema hivi:

      “Maiti za watu zitaanguka kama mbolea juu ya ardhi shambani,

      Kama safu ya miganda ya nafaka iliyotoka kukatwa na mvunaji,

      Bila mtu wa kuikusanya.”’”+

  • Yeremia 36:30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Kwa hiyo Yehova anasema hivi dhidi ya Mfalme Yehoyakimu wa Yuda, ‘Hatakuwa na mtu yeyote atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha Daudi,+ na maiti yake itaachwa nje kwenye joto wakati wa mchana na baridi kali wakati wa usiku.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki