Zaburi 79:2, 3 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 2 Wamewapa ndege wa angani maiti za watumishi wako kuwa chakula chaoNa miili ya washikamanifu wako wamewapa wanyama wa mwituni wa dunia.+ 3 Wamemwaga damu yao kama maji kotekote Yerusalemu,Na hakuna aliyebaki wa kuwazika.+ Isaya 5:25 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 25 Ndiyo sababu hasira ya Yehova inawaka dhidi ya watu wake,Naye ataunyoosha mkono wake dhidi yao na kuwapiga.+ Milima itatetemeka,Na maiti zao zitakuwa kama takataka barabarani.+ Kwa sababu ya hayo yote, hasira yake haijapoa,Lakini mkono wake bado umenyooshwa ili kupiga. Yeremia 7:33 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 33 Na maiti za watu hawa zitakuwa chakula cha ndege wa angani na cha wanyama wa duniani, na hakuna mtu atakayewafukuza.+ Yeremia 9:22 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 22 Sema, ‘Yehova anasema hivi: “Maiti za watu zitaanguka kama mbolea juu ya ardhi shambani,Kama safu ya miganda ya nafaka iliyotoka kukatwa na mvunaji,Bila mtu wa kuikusanya.”’”+ Yeremia 36:30 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 30 Kwa hiyo Yehova anasema hivi dhidi ya Mfalme Yehoyakimu wa Yuda, ‘Hatakuwa na mtu yeyote atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha Daudi,+ na maiti yake itaachwa nje kwenye joto wakati wa mchana na baridi kali wakati wa usiku.+
2 Wamewapa ndege wa angani maiti za watumishi wako kuwa chakula chaoNa miili ya washikamanifu wako wamewapa wanyama wa mwituni wa dunia.+ 3 Wamemwaga damu yao kama maji kotekote Yerusalemu,Na hakuna aliyebaki wa kuwazika.+
25 Ndiyo sababu hasira ya Yehova inawaka dhidi ya watu wake,Naye ataunyoosha mkono wake dhidi yao na kuwapiga.+ Milima itatetemeka,Na maiti zao zitakuwa kama takataka barabarani.+ Kwa sababu ya hayo yote, hasira yake haijapoa,Lakini mkono wake bado umenyooshwa ili kupiga.
33 Na maiti za watu hawa zitakuwa chakula cha ndege wa angani na cha wanyama wa duniani, na hakuna mtu atakayewafukuza.+
22 Sema, ‘Yehova anasema hivi: “Maiti za watu zitaanguka kama mbolea juu ya ardhi shambani,Kama safu ya miganda ya nafaka iliyotoka kukatwa na mvunaji,Bila mtu wa kuikusanya.”’”+
30 Kwa hiyo Yehova anasema hivi dhidi ya Mfalme Yehoyakimu wa Yuda, ‘Hatakuwa na mtu yeyote atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha Daudi,+ na maiti yake itaachwa nje kwenye joto wakati wa mchana na baridi kali wakati wa usiku.+