Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 24:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Kisha Yehoyakimu akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake;+ na Yehoyakini mwanawe akawa mfalme baada yake.

  • 2 Wafalme 24:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Yehoyakini+ alikuwa na umri wa miaka 18 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miezi mitatu huko Yerusalemu.+ Mama yake aliitwa Nehushta binti ya Elnathani wa Yerusalemu.

  • 2 Wafalme 24:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Basi akampeleka Yehoyakini+ uhamishoni Babiloni;+ alimpeleka pia mama ya mfalme, wake za mfalme, maofisa wa makao yake, na viongozi wa nchi, akawapeleka uhamishoni Babiloni kutoka Yerusalemu.

  • 2 Mambo ya Nyakati 36:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Yehoyakini+ alikuwa na umri wa miaka 18 alipoanza kutawala, alitawala kwa miezi mitatu na siku kumi huko Yerusalemu; naye aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova.+ 10 Mwanzoni mwa mwaka,* Mfalme Nebukadneza aliagiza aletwe Babiloni,+ pamoja na vyombo vyenye thamani vya nyumba ya Yehova.+ Akamweka Sedekia ndugu ya baba yake kuwa mfalme wa Yuda na Yerusalemu.+

  • Yeremia 22:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 “‘Kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Yehova, ‘hata kama Konia*+ mwana wa Yehoyakimu,+ mfalme wa Yuda, angekuwa pete ya muhuri kwenye mkono wangu wa kuume, ningekung’oa kutoka hapo!

  • Yeremia 22:30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Yehova anasema hivi:

      ‘Andikeni kwamba mtu huyu hana mtoto,

      Kama mtu ambaye hatafanikiwa katika maisha yake,*

      Kwa maana hakuna yeyote kati ya wazao wake atakayefanikiwa

      Kuketi kwenye kiti cha ufalme cha Daudi na kutawala tena katika Yuda.’”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki