Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 17:13, 14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Yehova aliwaonya Waisraeli na watu wa Yuda tena na tena kupitia manabii wake wote na kila mwonaji,+ akisema: “Geukeni na kuacha njia zenu ovu!+ Shikeni amri zangu na maagizo yangu kulingana na sheria yote niliyowaamuru mababu zenu na ambayo niliwapa kupitia watumishi wangu manabii.” 14 Lakini hawakusikiliza, nao wakaendelea kuwa wakaidi kama* mababu zao ambao hawakudhihirisha imani katika Yehova Mungu wao.+

  • Yeremia 7:12-14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “‘Hata hivyo, sasa nendeni mahali pangu huko Shilo,+ ambapo mwanzoni nilifanya jina langu likae,+ na kuona nilivyopafanya kwa sababu ya uovu wa watu wangu Waisraeli.+ 13 Lakini mliendelea kufanya mambo hayo yote,’ asema Yehova, ‘na ingawa nilizungumza nanyi tena na tena,* hamkusikiliza.+ Niliendelea kuwaita, lakini hamkujibu.+ 14 Ndivyo nitakavyoitendea nyumba inayoitwa kwa jina langu,+ ambayo mnaitumaini,+ na mahali hapa ambapo niliwapa ninyi na mababu zenu, kama nilivyoitendea Shilo.+

  • Yeremia 25:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 “Tangu mwaka wa 13 wa utawala wa Yosia+ mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda, mpaka leo hii, miaka hii 23, neno la Yehova limenijia, nami niliendelea kuwaambia tena na tena,* lakini hamkusikiliza.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki