Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 26:33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 Nitawatawanya miongoni mwa mataifa,+ nitachomoa upanga nanyi mtakimbizwa;+ na nchi yenu itaharibiwa, na majiji yenu yatabaki ukiwa.+

  • 2 Wafalme 24:14, 15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Akawapeleka uhamishoni watu wote wa Yerusalemu, wakuu wote,+ mashujaa wote hodari, na kila fundi na mfua chuma*+—aliwapeleka uhamishoni watu 10,000. Hakuna yeyote aliyebaki isipokuwa watu maskini kabisa nchini.+ 15 Basi akampeleka Yehoyakini+ uhamishoni Babiloni;+ alimpeleka pia mama ya mfalme, wake za mfalme, maofisa wa makao yake, na viongozi wa nchi, akawapeleka uhamishoni Babiloni kutoka Yerusalemu.

  • 2 Wafalme 25:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Mfalme wa Babiloni aliwaua na kuwaangamiza huko Ribla katika nchi ya Hamathi.+ Hivyo watu wa Yuda wakaenda uhamishoni kutoka katika nchi yao.+

  • Yeremia 39:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi akawapeleka uhamishoni kule Babiloni watu waliobaki jijini, na wale waliojisalimisha kwake, na yeyote aliyebaki.

  • Yeremia 52:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Mfalme wa Babiloni aliwapiga na kuwaangamiza huko Ribla+ katika nchi ya Hamathi. Hivyo watu wa Yuda wakapelekwa uhamishoni kutoka katika nchi yao.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki