Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 17:10-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Wakaendelea kujisimamishia nguzo takatifu na miti mitakatifu*+ juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti wenye majani mengi;+ 11 nao walikuwa wakifukiza moshi wa dhabihu mahali pote pa juu kama yalivyofanya mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyapeleka uhamishoni kutoka mbele yao.+ Waliendelea kutenda maovu na kumkasirisha Yehova.

      12 Waliendelea kuabudu sanamu zenye kuchukiza,*+ ambazo Yehova alikuwa amewaambia hivi kuzihusu: “Msifanye hivyo!”+

  • Yeremia 2:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 ‘Kwa maana zamani niliivunja nira yako+

      Na kuzikata pingu zako.

      Lakini ulisema: “Mimi sitatumikia,”

      Kwa maana juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti wenye majani mengi+

      Ulilala ukiwa umejinyoosha, ukifanya ukahaba.+

  • Ezekieli 20:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Niliwaleta katika nchi niliyoapa kwamba ningewapatia.+ Walipoona vilima vyote virefu na miti yenye majani mengi,+ walianza kutoa dhabihu zao na matoleo yao yanayochukiza. Walitoa harufu inayopendeza* ya dhabihu zao na kumwaga matoleo yao ya vinywaji hapo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki