-
Isaya 11:11, 12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Siku hiyo Yehova ataunyoosha tena mkono wake, mara ya pili, ili kuwakomboa watu wake waliobaki kutoka Ashuru,+ kutoka Misri,+ kutoka Pathrosi,+ kutoka Kushi,+ kutoka Elamu,+ kutoka Shinari,*+ kutoka Hamathi, na kutoka katika visiwa vya bahari. 12 Atainua ishara* kwa ajili ya mataifa na kuwakusanya watu wa Israeli+ waliotawanywa, na watu wa Yuda waliotawanywa atawakusanya pamoja kutoka katika pembe nne za dunia.+
-
-
Isaya 43:5, 6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Usiogope, kwa maana nipo pamoja nawe.+
6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’+
Na kusini, ‘Usiwazuie.
Walete wanangu kutoka mbali, na mabinti wangu kutoka kwenye miisho ya dunia,+
-
Yeremia 23:7, 8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 “Hata hivyo, siku zinakuja,” asema Yehova, “wakati ambapo hawatasema tena, ‘Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, aliyewatoa watu wa Israeli nchini Misri!’+ 8 badala yake watasema, ‘Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, aliyewatoa na kuwarudisha wazao wa nyumba ya Israeli kutoka katika nchi ya kaskazini na kutoka katika nchi zote nilizowatawanya,’ nao watakaa katika nchi yao wenyewe.”+
-
-
-