-
Yeremia 27:6, 7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Na sasa mimi mwenyewe nimezitia nchi hizi zote mikononi mwa mtumishi wangu Mfalme Nebukadneza+ wa Babiloni; nimempa hata wanyama wa mwituni ili wamtumikie. 7 Mataifa yote yatamtumikia yeye na mwanawe na mjukuu wake mpaka wakati wa nchi yake utakapofika,+ wakati ambapo mataifa mengi na wafalme wakuu watamfanya kuwa mtumwa wao.’+
-
-
Zekaria 2:7-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 “Njoo, Ee Sayuni! Kimbia, wewe unayekaa na binti ya Babiloni.+ 8 Kwa maana hivi ndivyo anavyosema Yehova wa majeshi, ambaye baada ya kutukuzwa* amenituma kwa mataifa yaliyokuwa yakiwapora ninyi:+ ‘Yeyote anayewagusa ninyi anaigusa mboni ya jicho langu.*+ 9 Kwa maana sasa nitaupunga mkono wangu dhidi yao, nao watakuwa nyara kwa watumwa wao wenyewe.’+ Na hakika mtajua kwamba Yehova wa majeshi amenituma.
-