7 Ninyi wanafiki, kwa kufaa Isaya alitabiri kuwahusu aliposema:+8 ‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami. 9 Wao huniabudu bure, kwa maana wanafundisha amri za wanadamu kuwa mafundisho.’”+
23 “Ole wenu, waandishi na Mafarisayo wanafiki! kwa sababu mnatoa sehemu ya kumi ya mnanaa na dili na bizari,+ lakini mmepuuza mambo mazito zaidi ya Sheria, yaani, haki,+ rehema,+ na uaminifu. Mlipaswa kufanya mambo hayo, bila kupuuza yale mengine.+
42 Lakini ole wenu Mafarisayo, kwa sababu mnatoa sehemu ya kumi ya mnanaa na mchicha na kila aina ya mboga,+ lakini mnapuuza haki na kumpenda Mungu! Mlipaswa kufanya mambo hayo, bila kupuuza yale mengine.+