-
Marko 8:34, 35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
34 Sasa akauita umati na wanafunzi wake, akawaambia: “Mtu yeyote akitaka kunifuata, lazima ajikane mwenyewe, aubebe mti wake wa mateso* na aendelee kunifuata.+ 35 Kwa kuwa yeyote anayetaka kuokoa uhai wake ataupoteza,* lakini yeyote anayeupoteza uhai wake* kwa ajili yangu na kwa ajili ya habari njema atauokoa.+
-