Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 17:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 “Ondoka, nenda Sarefathi ya Sidoni, nawe ukae huko. Tazama! Nitamwamuru mjane fulani huko akupe chakula.”+ 10 Basi akainuka na kwenda Sarefathi. Alipofika kwenye lango la jiji, kulikuwa na mwanamke fulani mjane aliyekuwa akiokota kuni. Basi akamwita mwanamke huyo na kumwambia: “Tafadhali, niletee maji kidogo kwenye kikombe ninywe.”+

  • 1 Wafalme 17:20-23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Akamlilia Yehova kwa sauti akisema: “Ee Yehova Mungu wangu,+ je, unamdhuru pia mjane ninayekaa kwake kwa kumuua mwanawe?” 21 Kisha akajinyoosha juu ya mtoto huyo mara tatu na kumlilia Yehova kwa sauti akisema: “Ee Yehova Mungu wangu, tafadhali, acha uhai wa mtoto huyu umrudie.” 22 Yehova akasikiliza ombi la Eliya,+ na uhai wa mtoto huyo ukamrudia, akawa hai tena.+ 23 Eliya akamchukua mtoto huyo, akamleta chini kutoka katika kile chumba cha darini, akampa mama yake; Eliya akasema: “Tazama, mwana wako yuko hai.”+

  • 2 Wafalme 4:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Siku moja Elisha alienda Shunemu,+ na huko kulikuwa na mwanamke mmoja maarufu, mwanamke huyo akamsihi sana ale chakula huko.+ Na kila mara alipopita mahali hapo, alikuwa akiingia mahali hapo kula chakula.

  • 2 Wafalme 4:13-17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Kisha Elisha akamwambia Gehazi: “Tafadhali mwambie mwanamke huyu, ‘Umejitaabisha sana kwa ajili yetu.+ Tukufanyie nini?+ Je, ninaweza kuzungumza na mfalme+ au mkuu wa jeshi kwa niaba yako?’” Lakini mwanamke huyo akasema: “Ninaishi miongoni mwa watu wangu mwenyewe.” 14 Kwa hiyo Elisha akauliza: “Basi tumfanyie nini mwanamke huyu?” Gehazi akasema: “Kwa kweli, hana mwana,+ na mume wake ni mzee.” 15 Mara moja akasema: “Mwite.” Basi akamwita, akaja na kusimama mlangoni. 16 Kisha Elisha akasema: “Wakati huu, mwaka ujao, utakuwa ukimkumbatia mwana.”+ Lakini mwanamke huyo akasema: “La hasha, bwana wangu, mtu wa Mungu wa kweli! Usinidanganye mimi kijakazi wako.”

      17 Hata hivyo, mwanamke huyo akapata mimba na kuzaa mwana wakati huohuo mwaka uliofuata, kama Elisha alivyomwambia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki