-
1 Wafalme 17:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 “Ondoka, nenda Sarefathi ya Sidoni, nawe ukae huko. Tazama! Nitamwamuru mjane fulani huko akupe chakula.”+ 10 Basi akainuka na kwenda Sarefathi. Alipofika kwenye lango la jiji, kulikuwa na mwanamke fulani mjane aliyekuwa akiokota kuni. Basi akamwita mwanamke huyo na kumwambia: “Tafadhali, niletee maji kidogo kwenye kikombe ninywe.”+
-
-
1 Wafalme 17:20-23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Akamlilia Yehova kwa sauti akisema: “Ee Yehova Mungu wangu,+ je, unamdhuru pia mjane ninayekaa kwake kwa kumuua mwanawe?” 21 Kisha akajinyoosha juu ya mtoto huyo mara tatu na kumlilia Yehova kwa sauti akisema: “Ee Yehova Mungu wangu, tafadhali, acha uhai wa mtoto huyu umrudie.” 22 Yehova akasikiliza ombi la Eliya,+ na uhai wa mtoto huyo ukamrudia, akawa hai tena.+ 23 Eliya akamchukua mtoto huyo, akamleta chini kutoka katika kile chumba cha darini, akampa mama yake; Eliya akasema: “Tazama, mwana wako yuko hai.”+
-
-
2 Wafalme 4:13-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Kisha Elisha akamwambia Gehazi: “Tafadhali mwambie mwanamke huyu, ‘Umejitaabisha sana kwa ajili yetu.+ Tukufanyie nini?+ Je, ninaweza kuzungumza na mfalme+ au mkuu wa jeshi kwa niaba yako?’” Lakini mwanamke huyo akasema: “Ninaishi miongoni mwa watu wangu mwenyewe.” 14 Kwa hiyo Elisha akauliza: “Basi tumfanyie nini mwanamke huyu?” Gehazi akasema: “Kwa kweli, hana mwana,+ na mume wake ni mzee.” 15 Mara moja akasema: “Mwite.” Basi akamwita, akaja na kusimama mlangoni. 16 Kisha Elisha akasema: “Wakati huu, mwaka ujao, utakuwa ukimkumbatia mwana.”+ Lakini mwanamke huyo akasema: “La hasha, bwana wangu, mtu wa Mungu wa kweli! Usinidanganye mimi kijakazi wako.”
17 Hata hivyo, mwanamke huyo akapata mimba na kuzaa mwana wakati huohuo mwaka uliofuata, kama Elisha alivyomwambia.
-