Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 32:39
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 39 Sasa tazameni kwamba mimi—mimi ndiye,+

      Na hakuna miungu mingine ila mimi.+

      Mimi huua, nami hufanya kuwa hai.+

      Ninajeruhi,+ nami nitaponya,+

      Na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote kutoka mikononi mwangu.+

  • 1 Samweli 2:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Yehova huua, naye huhifadhi uhai;*

      Hushusha Kaburini,* naye hufufua.+

  • 2 Wafalme 4:32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Elisha alipoingia katika nyumba hiyo, mvulana huyo alikuwa amelala kwenye kitanda chake akiwa mfu.+

  • 2 Wafalme 4:34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 Kisha akapanda kitandani na kumlalia mtoto huyo, kinywa chake kikiwa juu ya kinywa cha mvulana huyo, macho yake juu ya macho yake, na viganja vyake juu ya viganja vyake, akaendelea kumlalia, na mwili wa mtoto huyo ukaanza kupata joto.+

  • 2 Wafalme 13:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Wanaume fulani walipokuwa wakimzika mtu, waliona kundi la wavamizi, kwa hiyo wakamtupa mara moja mtu huyo ndani ya kaburi la Elisha na kukimbia. Mtu huyo alipogusa mifupa ya Elisha, akafufuka+ na kusimama.

  • Luka 7:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Yule mfu akaketi akaanza kuongea, naye Yesu akamkabidhi kwa mama yake.+

  • Luka 8:54, 55
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 54 Lakini akamshika mkono na kumwita: “Mtoto, inuka!”+ 55 Roho+ yake ikarudi* naye akasimama mara moja,+ kisha Yesu akaagiza apewe chakula.

  • Yohana 5:28, 29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Msishangazwe na jambo hili, kwa maana saa inakuja ambayo wote walio katika makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake+ 29 na kutoka, wale waliotenda mema kwenye ufufuo wa uzima, na wale waliozoea kutenda maovu kwenye ufufuo wa hukumu.+

  • Yohana 11:44
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 44 Mtu huyo aliyekuwa amekufa akatoka, miguu na mikono yake ikiwa imefungwa kwa vitambaa, na uso wake ukiwa umefungwa kwa kitambaa. Yesu akawaambia: “Mfungueni, mmwache aende.”

  • Matendo 9:40, 41
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 40 Petro akaagiza kila mtu aende nje,+ akapiga magoti na kusali. Kisha akaugeukia ule mwili, akasema: “Tabitha, inuka!” Akafungua macho yake, na alipomwona Petro, akaketi.+ 41 Petro akamshika mkono na kumwinua, akawaita watakatifu na wajane, akamkabidhi kwao akiwa hai.+

  • Matendo 20:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Kijana aitwaye Eutiko alikuwa ameketi dirishani, naye akalala usingizi mzito Paulo alipokuwa akiongea, basi akalemewa na usingizi, akaanguka chini kutoka ghorofa ya tatu, akaokotwa akiwa amekufa. 10 Lakini Paulo akashuka kutoka ghorofani, akajitupa juu yake akamkumbatia+ na kusema: “Acheni kupiga kelele, kwa maana yuko hai.”*+

  • Waroma 14:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Kwa maana kwa kusudi hili Kristo alikufa na akawa hai tena, ili awe Bwana juu ya waliokufa na walio hai pia.+

  • Waebrania 11:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kwa imani, Abrahamu alipojaribiwa,+ ni kana kwamba alimtoa Isaka—mtu huyo aliyekuwa amezipokea ahadi kwa furaha alijaribu kumtoa mwana wake mzaliwa-pekee+—

  • Waebrania 11:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Lakini alifikia uamuzi kwamba Mungu angeweza kumfufua hata kutoka kwa wafu, naye alimpokea kutoka huko kwa njia ya mfano.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki