Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 32:39
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 39 Sasa tazameni kwamba mimi—mimi ndiye,+

      Na hakuna miungu mingine ila mimi.+

      Mimi huua, nami hufanya kuwa hai.+

      Ninajeruhi,+ nami nitaponya,+

      Na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote kutoka mikononi mwangu.+

  • Ayubu 14:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Laiti ungenificha Kaburini,*+

      Ungenificha mpaka hasira yako ipite,

      Laiti ungenipimia wakati hususa na kunikumbuka!+

  • Zaburi 30:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Ee Yehova, umeniinua* kutoka Kaburini.*+

      Ulifanya niendelee kuwa hai; uliniokoa nisizame shimoni.*+

  • Zaburi 49:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Lakini Mungu atanikomboa* kutoka katika nguvu za* Kaburi,*+

      Kwa maana atanishika. (Sela)

  • Zaburi 68:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Kwetu, Mungu wa kweli ni Mungu anayeokoa;+

      Na Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu huokoa kutoka katika kifo.+

  • Hosea 13:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Nitawakomboa kutoka katika nguvu za Kaburi;*

      Nitawaokoa kutoka katika kifo.+

      Ewe Kifo, yako wapi maumivu yako makali?*+

      Ewe Kaburi, yako wapi maangamizi yako?+

      Macho yangu yatazuiwa yasione huruma.

  • Yohana 11:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Martha akamwambia: “Ninajua atafufuka katika ufufuo+ siku ya mwisho.”

  • 1 Wakorintho 15:55
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 55 “Kifo, uko wapi ushindi wako? Kifo, uko wapi mchomo wako?”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki