-
Marko 3:31-35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
31 Mama yake na ndugu zake+ wakaja na kusimama nje, wakamtuma mtu akamwite.+ 32 Kwa kuwa umati ulikuwa umeketi kumzunguka, wakamwambia: “Tazama! Mama yako na ndugu zako wako nje wanakuita.”+ 33 Lakini akawauliza: “Mama yangu na ndugu zangu ni nani?” 34 Akawatazama watu walioketi kumzunguka, akasema: “Tazama, mama yangu na ndugu zangu!+ 35 Yeyote anayefanya mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu, dada yangu, na mama yangu.”+
-