-
Mathayo 12:46-50Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
46 Alipokuwa bado akizungumza na umati, mama yake na ndugu zake+ walikuwa wamesimama nje, wakitaka kuongea naye.+ 47 Basi mtu fulani akamwambia: “Tazama! Mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kuongea nawe.” 48 Yesu akamjibu mtu huyo: “Mama yangu ni nani, na ndugu zangu ni nani?” 49 Akinyoosha mkono wake kuelekea wanafunzi wake, akasema: “Tazama! Mama yangu na ndugu zangu!+ 50 Kwa maana yeyote anayefanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, dada yangu, na mama yangu.”+
-