48 Yesu akamjibu mtu huyo: “Mama yangu ni nani, na ndugu zangu ni nani?” 49 Akinyoosha mkono wake kuelekea wanafunzi wake, akasema: “Tazama! Mama yangu na ndugu zangu!+ 50 Kwa maana yeyote anayefanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, dada yangu, na mama yangu.”+