Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wakorintho 2:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Lakini kama ilivyoandikwa: “Jicho halijaona na sikio halijasikia, wala hayajawaziwa katika moyo wa mwanadamu mambo ambayo Mungu amewatayarishia wale wanaompenda.”+ 10 Kwa maana Mungu ameyafunua kwetu+ kupitia roho yake,+ kwa maana roho huchunguza ndani ya mambo yote, hata mambo mazito* ya Mungu.+

  • Waefeso 1:9-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 kwa kutujulisha siri takatifu+ ya mapenzi yake. Ni kulingana na mapenzi yake mema aliyokusudia mwenyewe 10 kwa ajili ya usimamizi* kwenye nyakati kamili zilizowekwa, kukusanya pamoja vitu vyote katika Kristo, vitu vilivyo mbinguni na vitu vilivyo duniani.+ Ndiyo, katika yeye 11 ambaye tuko katika muungano naye na tulihesabiwa kuwa warithi,+ kwa kuwa tuliagizwa awali kulingana na kusudi la yule anayetimiza mambo yote kama anavyoamua kulingana na mapenzi yake, 12 ili sisi tulio wa kwanza kumtumaini Kristo tutumikie kwa ajili ya sifa ya utukufu wake.

  • Wakolosai 1:26, 27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 siri takatifu+ iliyokuwa imefichwa tangu mifumo ya mambo iliyopita*+ na tangu vizazi vilivyopita. Lakini sasa imefunuliwa kwa watakatifu wake,+ 27 ambao Mungu amependezwa kuwajulisha kati ya mataifa utajiri wenye utukufu wa hii siri takatifu,+ ambayo ni Kristo katika muungano nanyi, tumaini la utukufu wake.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki