Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Marko 6:1-6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Akaondoka huko na kwenda kwenye eneo lake la nyumbani,+ na wanafunzi wake wakamfuata. 2 Ilipofika siku ya Sabato, akaanza kufundisha katika sinagogi, na wengi waliomsikiliza wakashangaa na kusema: “Mtu huyu alitoa wapi mambo haya?+ Kwa nini alipewa hekima hii, na kwa nini matendo haya yenye nguvu yafanywe kupitia mikono yake?+ 3 Je, huyu si yule seremala+ mwana wa Maria+ na ndugu ya Yakobo,+ Yosefu, Yuda, na Simoni?+ Na dada zake wapo hapa pamoja nasi, sivyo?” Basi wakaanza kukwazika kwa sababu yake. 4 Lakini Yesu akawaambia: “Nabii anaheshimiwa kila mahali isipokuwa katika eneo lake la nyumbani na kati ya watu wake wa ukoo, na katika nyumba yake mwenyewe.”+ 5 Basi, hakuweza kufanya matendo yoyote yenye nguvu huko isipokuwa kuweka mikono yake juu ya wagonjwa wachache na kuwaponya. 6 Kwa kweli, alishangaa sana kwa sababu hawakuwa na imani. Naye akaenda akizunguka vijijini, akifundisha.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki