-
Marko 6:1-6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Akaondoka huko na kwenda kwenye eneo lake la nyumbani,+ na wanafunzi wake wakamfuata. 2 Ilipofika siku ya Sabato, akaanza kufundisha katika sinagogi, na wengi waliomsikiliza wakashangaa na kusema: “Mtu huyu alitoa wapi mambo haya?+ Kwa nini alipewa hekima hii, na kwa nini matendo haya yenye nguvu yafanywe kupitia mikono yake?+ 3 Je, huyu si yule seremala+ mwana wa Maria+ na ndugu ya Yakobo,+ Yosefu, Yuda, na Simoni?+ Na dada zake wapo hapa pamoja nasi, sivyo?” Basi wakaanza kukwazika kwa sababu yake. 4 Lakini Yesu akawaambia: “Nabii anaheshimiwa kila mahali isipokuwa katika eneo lake la nyumbani na kati ya watu wake wa ukoo, na katika nyumba yake mwenyewe.”+ 5 Basi, hakuweza kufanya matendo yoyote yenye nguvu huko isipokuwa kuweka mikono yake juu ya wagonjwa wachache na kuwaponya. 6 Kwa kweli, alishangaa sana kwa sababu hawakuwa na imani. Naye akaenda akizunguka vijijini, akifundisha.+
-