-
Mathayo 13:54-58Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
54 Baada ya kuingia katika eneo lake la nyumbani,+ akaanza kuwafundisha katika sinagogi lao, hivi kwamba wakashangaa na kuuliza: “Mtu huyu alipata wapi hekima hii na matendo haya yenye nguvu?+ 55 Je, huyu si mwana wa yule seremala?+ Je, mama yake haitwi Maria, na ndugu zake Yakobo, Yosefu, Simoni, na Yuda?+ 56 Na dada zake, je, wote hawako pamoja nasi? Basi, alipata wapi mambo haya yote?”+ 57 Kwa hiyo, wakaanza kukwazika kwa sababu yake.+ Lakini Yesu akawaambia: “Nabii anaheshimiwa kila mahali isipokuwa katika eneo lake la nyumbani na katika nyumba yake mwenyewe.”+ 58 Naye hakufanya matendo mengi yenye nguvu huko kwa sababu hawakuwa na imani.
-