-
Yohana 2:14-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 Alipoingia hekaluni akakuta watu wakiuza ng’ombe, kondoo, na njiwa,+ pia, wale waliobadili pesa walikuwa kwenye viti vyao. 15 Basi akatengeneza mjeledi wa kamba na kuwafukuza hekaluni wote waliokuwa na kondoo na ng’ombe, akamwaga sarafu za wale waliobadili pesa na kupindua meza zao.+ 16 Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa: “Ondoeni vitu hivi hapa! Acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara!”*+
-