Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 103:10-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Hajatutendea kulingana na dhambi zetu,+

      Wala hajatupa adhabu tuliyostahili kulingana na makosa yetu.+

      11 Kwa maana kama mbingu zilivyo juu kuliko dunia,

      Ndivyo upendo wake mshikamanifu ulivyo mkubwa kuelekea wale wanaomwogopa.+

      12 Kama mashariki ilivyo mbali sana na magharibi,

      Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali sana na sisi.+

  • Mathayo 6:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 na utusamehe madeni yetu, kama vile tunavyowasamehe wadeni wetu.+

  • Mathayo 6:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 “Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia;+

  • Waefeso 4:32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Bali mtendeane kwa fadhili, huruma nyororo,+ mkisameheana kwa hiari kama vile Mungu alivyowasamehe ninyi kwa hiari kupitia Kristo.+

  • Wakolosai 3:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Endeleeni kuvumiliana na kusameheana kwa hiari+ hata ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika juu ya mwingine.+ Kama vile Yehova* alivyowasamehe kwa hiari, nanyi lazima mfanye vivyo hivyo.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki