-
Mathayo 27:33-37Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
33 Na walipofika mahali panapoitwa Golgotha, yaani, Mahali pa Fuvu la Kichwa,+ 34 wakampa divai iliyochanganywa na nyongo* anywe;+ lakini alipoionja, akakataa kuinywa. 35 Baada ya kumtundika kwenye mti, wakagawana mavazi yake ya nje kwa kupiga kura,+ 36 kisha wakaketi hapo wakimlinda. 37 Pia, wakabandika juu ya kichwa chake mashtaka dhidi yake, yalikuwa yameandikwa: “Huyu ni Yesu Mfalme wa Wayahudi.”+
-