Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 9:23-26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Basi alipoingia katika nyumba ya yule mtawala na kuwaona watu waliokuwa wakipiga filimbi na umati uliokuwa na vurugu,+ 24 Yesu akasema: “Ondokeni hapa, kwa maana msichana huyu mdogo hajafa bali amelala usingizi.”+ Ndipo wakaanza kumcheka kwa dharau. 25 Mara tu umati ulipoondolewa, Yesu akaingia na kumshika mkono,+ kisha yule msichana mdogo akainuka.+ 26 Bila shaka, habari hiyo ilienea katika eneo hilo lote.

  • Marko 5:38-43
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 38 Wakafika kwenye nyumba ya yule ofisa msimamizi wa sinagogi, Yesu akaona mvurugo wa watu waliokuwa wakilia na kuomboleza kwa sauti kubwa.+ 39 Baada ya kuingia, akawaambia: “Kwa nini mnaomboleza na kuleta mvurugo? Mtoto hajafa bali amelala usingizi.”+ 40 Ndipo wakaanza kumcheka kwa dharau. Lakini baada ya kuwatoa wote nje, akamchukua baba na mama ya yule mtoto pamoja na wanafunzi wake, akaingia mahali alipokuwa huyo mtoto. 41 Kisha akaushika mkono wa msichana huyo na kumwambia: “Talitha kumi,” maneno ambayo yanapotafsiriwa, yanamaanisha: “Msichana mdogo, ninakuambia, ‘inuka!’”+ 42 Mara moja yule msichana akasimama akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka 12.) Ndipo wakawa na shangwe kubwa sana. 43 Lakini akawaagiza tena na tena* wasimwambie mtu yeyote kuhusu jambo hilo,+ naye akawaambia wampe mtoto huyo chakula.

  • Yohana 11:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Baada ya kusema hayo, akawaambia: “Rafiki yetu Lazaro amelala usingizi,+ lakini ninasafiri kwenda huko ili kumwamsha.”

  • Matendo 7:60
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 60 Kisha akapiga magoti, akasema kwa sauti kubwa: “Yehova,* usiwahesabie dhambi hii.”+ Na baada ya kusema hayo, akalala usingizi katika kifo.

  • Matendo 13:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Kwa upande wake, Daudi alimtumikia Mungu* katika kizazi chake mwenyewe, akalala usingizi katika kifo, akazikwa pamoja na mababu zake, naye akaona uharibifu.*+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki