-
Marko 5:38-43Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
38 Wakafika kwenye nyumba ya yule ofisa msimamizi wa sinagogi, Yesu akaona mvurugo wa watu waliokuwa wakilia na kuomboleza kwa sauti kubwa.+ 39 Baada ya kuingia, akawaambia: “Kwa nini mnaomboleza na kuleta mvurugo? Mtoto hajafa bali amelala usingizi.”+ 40 Ndipo wakaanza kumcheka kwa dharau. Lakini baada ya kuwatoa wote nje, akamchukua baba na mama ya yule mtoto pamoja na wanafunzi wake, akaingia mahali alipokuwa huyo mtoto. 41 Kisha akaushika mkono wa msichana huyo na kumwambia: “Talitha kumi,” maneno ambayo yanapotafsiriwa, yanamaanisha: “Msichana mdogo, ninakuambia, ‘inuka!’”+ 42 Mara moja yule msichana akasimama akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka 12.) Ndipo wakawa na shangwe kubwa sana. 43 Lakini akawaagiza tena na tena* wasimwambie mtu yeyote kuhusu jambo hilo,+ naye akawaambia wampe mtoto huyo chakula.
-
-
Luka 8:52-56Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
52 Lakini watu wote walikuwa wakilia na kujipigapiga kwa huzuni kwa sababu ya yule msichana. Basi akawaambia: “Acheni kulia,+ kwa maana hajafa bali amelala usingizi.”+ 53 Ndipo wakaanza kumcheka kwa dharau, kwa sababu walijua amekufa. 54 Lakini akamshika mkono na kumwita: “Mtoto, inuka!”+ 55 Roho+ yake ikarudi* naye akasimama mara moja,+ kisha Yesu akaagiza apewe chakula. 56 Basi, wazazi wake wakafurahi sana, lakini Yesu akawaagiza wasimwambie mtu yeyote kilichotukia.+
-